Psalms 83:1-6

Maombi Kwa Ajili Ya Kushindwa Kwa Adui Wa Israeli

(Zaburi Ya Asafu. Wimbo)


1 aEe Mungu, usinyamaze kimya,
usinyamaze, Ee Mungu, usitulie.

2 bTazama watesi wako wanafanya fujo,
jinsi adui zako wanavyoinua vichwa vyao.

3 cKwa hila, wanafanya shauri dhidi ya watu wako,
wanafanya shauri baya dhidi ya wale unaowapenda.

4 dWanasema, “Njooni, tuwaangamize kama taifa,
ili jina la Israeli lisikumbukwe tena.”


5 eKwa nia moja wanapanga mashauri mabaya pamoja,
wanafanya muungano dhidi yako,

6 fmahema ya Edomu na Waishmaeli,
ya Wamoabu na Wahagari,
Copyright information for SwhKC