Psalms 83:1-6
Maombi Kwa Ajili Ya Kushindwa Kwa Adui Wa Israeli
(Zaburi Ya Asafu. Wimbo)
1 aEe Mungu, usinyamaze kimya,
usinyamaze, Ee Mungu, usitulie.
2 bTazama watesi wako wanafanya fujo,
jinsi adui zako wanavyoinua vichwa vyao.
3 cKwa hila, wanafanya shauri dhidi ya watu wako,
wanafanya shauri baya dhidi ya wale unaowapenda.
4 dWanasema, “Njooni, tuwaangamize kama taifa,
ili jina la Israeli lisikumbukwe tena.”
5 eKwa nia moja wanapanga mashauri mabaya pamoja,
wanafanya muungano dhidi yako,
6 fmahema ya Edomu na Waishmaeli,
ya Wamoabu na Wahagari,
Copyright information for
SwhKC